logo
HARUN YAHYA
  • 1. Litakapo tukia hilo Tukio
  • 2. Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
  • 3. Literemshalo linyanyualo,
  • 4. Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
  • 5. Na milima itapo sagwasagwa,
  • 6. Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
  • 7. Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
  • 8. Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
  • 9. Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
  • 10. Na wa mbele watakuwa mbele.
  • 11. Hao ndio watakao karibishwa
  • 12. Katika Bustani zenye neema.
  • 13. Fungu kubwa katika wa mwanzo,
  • 14. Na wachache katika wa mwisho.
  • 15. Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
  • 16. Wakiviegemea wakielekeana.
  • 17. Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
  • 18. Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
  • 19. Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
  • 20. Na matunda wayapendayo,
  • 21. Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
  • 22. Na Mahurulaini,
  • 23. Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
  • 24. Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
  • 25. Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
  • 26. Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
  • 27. Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
  • 28. Katika mikunazi isiyo na miba,
  • 29. Na migomba iliyo pangiliwa,
  • 30. Na kivuli kilicho tanda,
  • 31. Na maji yanayo miminika,
  • 32. Na matunda mengi,
  • 33. Hayatindikii wala hayakatazwi,
  • 34. Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
  • 35. Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
  • 36. Na tutawafanya vijana,
  • 37. Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
  • 38. Kwa ajili ya watu wa kuliani.
  • 39. Fungu kubwa katika wa mwanzo,
  • 40. Na fungu kubwa katika wa mwisho.
  • 41. Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
  • 42. Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
  • 43. Na kivuli cha moshi mweusi,
  • 44. Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
  • 45. Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
  • 46. Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
  • 47. Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
  • 48. Au baba zetu wa zamani?
  • 49. Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
  • 50. Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
  • 51. Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
  • 52. Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
  • 53. Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
  • 54. Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
  • 55. Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
  • 56. Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
  • 57. Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
  • 58. Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
  • 59. Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
  • 60. Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
  • 61. Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
  • 62. Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
  • 63. Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
  • 64. Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
  • 65. Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
  • 66. Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
  • 67. Bali sisi tumenyimwa.
  • 68. Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
  • 69. Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
  • 70. Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
  • 71. Je! Mnauona moto mnao uwasha?
  • 72. Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
  • 73. Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
  • 74. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
  • 75. Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
  • 76. Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
  • 77. Hakika hii bila ya shaka ni Qur`ani Tukufu,
  • 78. Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
  • 79. Hapana akigusaye ila walio takaswa.
  • 80. Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
  • 81. Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
  • 82. Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
  • 83. Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
  • 84. Na nyinyi wakati huo mnatazama!
  • 85. Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
  • 86. Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
  • 87. Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
  • 88. Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
  • 89. Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
  • 90. Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
  • 91. Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
  • 92. Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
  • 93. Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
  • 94. Na kutiwa Motoni.
  • 95. Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
  • 96. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
SHIRIKI
logo
logo
logo
logo
logo
  • 1.Al-Fatihah
  • 2.Al Baqara
  • 3.Ali `Imran
  • 4.An-Nisa
  • 5.Al-Ma`idah
  • 6.Al-An`am
  • 7.Al-A`raf
  • 8.Al-Anfal
  • 9.At-Tawbah
  • 10.Yunus
  • 11.Hud
  • 12.Yusuf
  • 13.Ar-Ra`d
  • 14.Ibrahim
  • 15.Al-Hijr
  • 16.An-Nahl
  • 17.Al-Isra
  • 18.Al-Kahf
  • 19.Maryam
  • 20.Taha
  • 21.Al-Anbya
  • 22.Al-Haj
  • 23.Al-Mu`minun
  • 24.An-Nur
  • 25.Al-Furqan
  • 26.Ash-Shu`ara
  • 27.An-Naml
  • 28.Al-Qasas
  • 29.Al-`Ankabut
  • 30.Ar-Rum
  • 31.Luqman
  • 32.As-Sajdah
  • 33.Al-Ahzab
  • 34.Saba
  • 35.Faatir
  • 36.Ya-Sin
  • 37.As-Saffat
  • 38.Sad
  • 39.Az-Zumar
  • 40.Ghafir
  • 41.Fussilat
  • 42.sh-Shuraa
  • 43.Az-Zukhruf
  • 44.Ad-Dukhan
  • 45.Al-Jathiyah
  • 46.Al-Ahqaf
  • 47.Muhammad
  • 48.Al-Fath
  • 49.Al-Hujurat
  • 50.Qaf
  • 51.Adh-Dhariyat
  • 52.At-Tur
  • 53.An-Najm
  • 54.Al-Qamar
  • 55.Ar-Rahman
  • 56.Al-Waqi`ah
  • 57.Al-Hadid
  • 58.Al-Mujadila
  • 59.Al-Hashr
  • 60.Al-Mumtahanah
  • 61.As-Saf
  • 62.Al-Jumu`ah
  • 63.Al-Munafiqun
  • 64.At-Taghabun
  • 65.At-Talaq
  • 66.At-Tahrim
  • 67.Al-Mulk
  • 68.Al-Qalam
  • 69.Al-Haqqah
  • 70.Al-Ma`arij
  • 71.Nuh
  • 72.Al-Jinn
  • 73.Al-Muzzammil
  • 74.Al-Muddaththir
  • 75.Al-Qiyamah
  • 76.Al-Insan
  • 77.Al-Mursalat
  • 78.An-Naba
  • 79.An-Nazi`at
  • 80.Abasa
  • 81.At-Takwir
  • 82.Al-Infitar
  • 83.Al-Mutaffifin
  • 84.Al-Inshiqaq
  • 85.Al-Buruj
  • 86.At-Tariq
  • 87.Al-A`la
  • 88.Al-Ghashiyah
  • 89.Al-Fajr
  • 90.Al-Balad
  • 91.Ash-Shams
  • 92.Al-Layl
  • 93.Ad-Duhaa
  • 94.Ash-Sharh
  • 95.At-Tin
  • 96.Al-`Alaq
  • 97.Al-Qadr
  • 98.Al-Bayyinah
  • 99.Az-Zalzalah
  • 100.Al-`Adiyat
  • 101.Al-Qari`ah
  • 102.At-Takathur
  • 103.Al-`Asr
  • 104.Al-Humazah
  • 105.Al-Fil
  • 106.Quraysh
  • 107.Al-Ma`un
  • 108.Al-Kawthar
  • 109.Al-Kafirun
  • 110.An-Nasr
  • 111.Al-Masad
  • 112.Al-Ikhlas
  • 113.Al-Falaq
  • 114.An-Nas