logo
HARUN YAHYA
  • 1. Naapa kwa mlima wa T`ur,
  • 2. Na Kitabu kilicho andikwa
  • 3. Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
  • 4. Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
  • 5. Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
  • 6. Na kwa bahari iliyo jazwa,
  • 7. Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
  • 8. Hapana wa kuizuia.
  • 9. Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
  • 10. Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
  • 11. Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
  • 12. Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
  • 13. Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
  • 14. (Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
  • 15. Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
  • 16. Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
  • 17. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
  • 18. Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
  • 19. Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
  • 20. Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
  • 21. Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
  • 22. Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
  • 23. Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
  • 24. Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
  • 25. Wataelekeana wakiulizana.
  • 26. Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
  • 27. Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
  • 28. Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
  • 29. Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
  • 30. Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
  • 31. Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
  • 32. Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
  • 33. Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
  • 34. Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
  • 35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
  • 36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
  • 37. Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
  • 38. Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
  • 39. Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
  • 40. Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
  • 41. Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
  • 42. Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
  • 43. Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
  • 44. Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
  • 45. Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
  • 46. Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
  • 47. Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
  • 48. Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
  • 49. Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
SHIRIKI
logo
logo
logo
logo
logo
  • 1.Al-Fatihah
  • 2.Al Baqara
  • 3.Ali `Imran
  • 4.An-Nisa
  • 5.Al-Ma`idah
  • 6.Al-An`am
  • 7.Al-A`raf
  • 8.Al-Anfal
  • 9.At-Tawbah
  • 10.Yunus
  • 11.Hud
  • 12.Yusuf
  • 13.Ar-Ra`d
  • 14.Ibrahim
  • 15.Al-Hijr
  • 16.An-Nahl
  • 17.Al-Isra
  • 18.Al-Kahf
  • 19.Maryam
  • 20.Taha
  • 21.Al-Anbya
  • 22.Al-Haj
  • 23.Al-Mu`minun
  • 24.An-Nur
  • 25.Al-Furqan
  • 26.Ash-Shu`ara
  • 27.An-Naml
  • 28.Al-Qasas
  • 29.Al-`Ankabut
  • 30.Ar-Rum
  • 31.Luqman
  • 32.As-Sajdah
  • 33.Al-Ahzab
  • 34.Saba
  • 35.Faatir
  • 36.Ya-Sin
  • 37.As-Saffat
  • 38.Sad
  • 39.Az-Zumar
  • 40.Ghafir
  • 41.Fussilat
  • 42.sh-Shuraa
  • 43.Az-Zukhruf
  • 44.Ad-Dukhan
  • 45.Al-Jathiyah
  • 46.Al-Ahqaf
  • 47.Muhammad
  • 48.Al-Fath
  • 49.Al-Hujurat
  • 50.Qaf
  • 51.Adh-Dhariyat
  • 52.At-Tur
  • 53.An-Najm
  • 54.Al-Qamar
  • 55.Ar-Rahman
  • 56.Al-Waqi`ah
  • 57.Al-Hadid
  • 58.Al-Mujadila
  • 59.Al-Hashr
  • 60.Al-Mumtahanah
  • 61.As-Saf
  • 62.Al-Jumu`ah
  • 63.Al-Munafiqun
  • 64.At-Taghabun
  • 65.At-Talaq
  • 66.At-Tahrim
  • 67.Al-Mulk
  • 68.Al-Qalam
  • 69.Al-Haqqah
  • 70.Al-Ma`arij
  • 71.Nuh
  • 72.Al-Jinn
  • 73.Al-Muzzammil
  • 74.Al-Muddaththir
  • 75.Al-Qiyamah
  • 76.Al-Insan
  • 77.Al-Mursalat
  • 78.An-Naba
  • 79.An-Nazi`at
  • 80.Abasa
  • 81.At-Takwir
  • 82.Al-Infitar
  • 83.Al-Mutaffifin
  • 84.Al-Inshiqaq
  • 85.Al-Buruj
  • 86.At-Tariq
  • 87.Al-A`la
  • 88.Al-Ghashiyah
  • 89.Al-Fajr
  • 90.Al-Balad
  • 91.Ash-Shams
  • 92.Al-Layl
  • 93.Ad-Duhaa
  • 94.Ash-Sharh
  • 95.At-Tin
  • 96.Al-`Alaq
  • 97.Al-Qadr
  • 98.Al-Bayyinah
  • 99.Az-Zalzalah
  • 100.Al-`Adiyat
  • 101.Al-Qari`ah
  • 102.At-Takathur
  • 103.Al-`Asr
  • 104.Al-Humazah
  • 105.Al-Fil
  • 106.Quraysh
  • 107.Al-Ma`un
  • 108.Al-Kawthar
  • 109.Al-Kafirun
  • 110.An-Nasr
  • 111.Al-Masad
  • 112.Al-Ikhlas
  • 113.Al-Falaq
  • 114.An-Nas