logo
HARUN YAHYA
  • 1. Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
  • 2. Na zinazo beba mizigo,
  • 3. Na zinazo kwenda kwa wepesi.
  • 4. Na zinazo gawanya kwa amri,
  • 5. Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
  • 6. Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
  • 7. Naapa kwa mbingu zenye njia,
  • 8. Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
  • 9. Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
  • 10. Wazushi wameangamizwa.
  • 11. Ambao wameghafilika katika ujinga.
  • 12. Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
  • 13. Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
  • 14. Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
  • 15. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
  • 16. Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
  • 17. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
  • 18. Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
  • 19. Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
  • 20. Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
  • 21. Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
  • 22. Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
  • 23. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
  • 24. Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
  • 25. Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
  • 26. Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
  • 27. Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
  • 28. Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
  • 29. Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
  • 30. Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
  • 31. AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
  • 32. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
  • 33. Tuwatupie mawe ya udongo,
  • 34. Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
  • 35. Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
  • 36. Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
  • 37. Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
  • 38. Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
  • 39. Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
  • 40. Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
  • 41. Na katika khabari za A`di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
  • 42. Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
  • 43. Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
  • 44. Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
  • 45. Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
  • 46. Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
  • 47. Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
  • 48. Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
  • 49. Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
  • 50. Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
  • 51. Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
  • 52. Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
  • 53. Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
  • 54. Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
  • 55. Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
  • 56. Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
  • 57. Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
  • 58. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
  • 59. Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
  • 60. Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
SHIRIKI
logo
logo
logo
logo
logo
  • 1.Al-Fatihah
  • 2.Al Baqara
  • 3.Ali `Imran
  • 4.An-Nisa
  • 5.Al-Ma`idah
  • 6.Al-An`am
  • 7.Al-A`raf
  • 8.Al-Anfal
  • 9.At-Tawbah
  • 10.Yunus
  • 11.Hud
  • 12.Yusuf
  • 13.Ar-Ra`d
  • 14.Ibrahim
  • 15.Al-Hijr
  • 16.An-Nahl
  • 17.Al-Isra
  • 18.Al-Kahf
  • 19.Maryam
  • 20.Taha
  • 21.Al-Anbya
  • 22.Al-Haj
  • 23.Al-Mu`minun
  • 24.An-Nur
  • 25.Al-Furqan
  • 26.Ash-Shu`ara
  • 27.An-Naml
  • 28.Al-Qasas
  • 29.Al-`Ankabut
  • 30.Ar-Rum
  • 31.Luqman
  • 32.As-Sajdah
  • 33.Al-Ahzab
  • 34.Saba
  • 35.Faatir
  • 36.Ya-Sin
  • 37.As-Saffat
  • 38.Sad
  • 39.Az-Zumar
  • 40.Ghafir
  • 41.Fussilat
  • 42.sh-Shuraa
  • 43.Az-Zukhruf
  • 44.Ad-Dukhan
  • 45.Al-Jathiyah
  • 46.Al-Ahqaf
  • 47.Muhammad
  • 48.Al-Fath
  • 49.Al-Hujurat
  • 50.Qaf
  • 51.Adh-Dhariyat
  • 52.At-Tur
  • 53.An-Najm
  • 54.Al-Qamar
  • 55.Ar-Rahman
  • 56.Al-Waqi`ah
  • 57.Al-Hadid
  • 58.Al-Mujadila
  • 59.Al-Hashr
  • 60.Al-Mumtahanah
  • 61.As-Saf
  • 62.Al-Jumu`ah
  • 63.Al-Munafiqun
  • 64.At-Taghabun
  • 65.At-Talaq
  • 66.At-Tahrim
  • 67.Al-Mulk
  • 68.Al-Qalam
  • 69.Al-Haqqah
  • 70.Al-Ma`arij
  • 71.Nuh
  • 72.Al-Jinn
  • 73.Al-Muzzammil
  • 74.Al-Muddaththir
  • 75.Al-Qiyamah
  • 76.Al-Insan
  • 77.Al-Mursalat
  • 78.An-Naba
  • 79.An-Nazi`at
  • 80.Abasa
  • 81.At-Takwir
  • 82.Al-Infitar
  • 83.Al-Mutaffifin
  • 84.Al-Inshiqaq
  • 85.Al-Buruj
  • 86.At-Tariq
  • 87.Al-A`la
  • 88.Al-Ghashiyah
  • 89.Al-Fajr
  • 90.Al-Balad
  • 91.Ash-Shams
  • 92.Al-Layl
  • 93.Ad-Duhaa
  • 94.Ash-Sharh
  • 95.At-Tin
  • 96.Al-`Alaq
  • 97.Al-Qadr
  • 98.Al-Bayyinah
  • 99.Az-Zalzalah
  • 100.Al-`Adiyat
  • 101.Al-Qari`ah
  • 102.At-Takathur
  • 103.Al-`Asr
  • 104.Al-Humazah
  • 105.Al-Fil
  • 106.Quraysh
  • 107.Al-Ma`un
  • 108.Al-Kawthar
  • 109.Al-Kafirun
  • 110.An-Nasr
  • 111.Al-Masad
  • 112.Al-Ikhlas
  • 113.Al-Falaq
  • 114.An-Nas