logo
HARUN YAHYA
  • 1. Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur`ani inayo bainisha.
  • 2. HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
  • 3. Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
  • 4. Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
  • 5. Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
  • 6. Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
  • 7. Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
  • 8. Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
  • 9. Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
  • 10. Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
  • 11. Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
  • 12. Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
  • 13. Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
  • 14. Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
  • 15. Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
  • 16. Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
  • 17. Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
  • 18. Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
  • 19. Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
  • 20. Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
  • 21. Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
  • 22. Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
  • 23. Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
  • 24. Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
  • 25. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
  • 26. Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
  • 27. Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
  • 28. Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
  • 29. Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
  • 30. Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
  • 31. Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
  • 32. (Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
  • 33. Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
  • 34. (Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
  • 35. Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
  • 36. Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
  • 37. (Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
  • 38. Mpaka siku ya wakati maalumu.
  • 39. Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
  • 40. Ila waja wako walio safika.
  • 41. Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
  • 42. Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
  • 43. Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
  • 44. Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
  • 45. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
  • 46. (Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
  • 47. Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
  • 48. Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
  • 49. Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
  • 50. Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
  • 51. Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
  • 52. Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
  • 53. Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
  • 54. Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
  • 55. Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
  • 56. Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
  • 57. Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
  • 58. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
  • 59. Isipo kuwa walio mfuata Luut`i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
  • 60. Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
  • 61. Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut`i,
  • 62. Alisema (Luut`i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
  • 63. Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
  • 64. Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
  • 65. Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
  • 66. Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
  • 67. Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
  • 68. Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
  • 69. Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
  • 70. Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
  • 71. Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
  • 72. Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
  • 73. Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
  • 74. Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
  • 75. Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
  • 76. Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
  • 77. Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
  • 78. Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
  • 79. Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
  • 80. Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
  • 81. Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
  • 82. Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
  • 83. Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
  • 84. Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
  • 85. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
  • 86. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
  • 87. Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur`ani Tukufu.
  • 88. Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
  • 89. Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
  • 90. Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
  • 91. Ambao wakaifanya Qur`ani vipande vipande.
  • 92. Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
  • 93. Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
  • 94. Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
  • 95. Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
  • 96. Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
  • 97. Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
  • 98. Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
  • 99. Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
SHIRIKI
logo
logo
logo
logo
logo
  • 1.Al-Fatihah
  • 2.Al Baqara
  • 3.Ali `Imran
  • 4.An-Nisa
  • 5.Al-Ma`idah
  • 6.Al-An`am
  • 7.Al-A`raf
  • 8.Al-Anfal
  • 9.At-Tawbah
  • 10.Yunus
  • 11.Hud
  • 12.Yusuf
  • 13.Ar-Ra`d
  • 14.Ibrahim
  • 15.Al-Hijr
  • 16.An-Nahl
  • 17.Al-Isra
  • 18.Al-Kahf
  • 19.Maryam
  • 20.Taha
  • 21.Al-Anbya
  • 22.Al-Haj
  • 23.Al-Mu`minun
  • 24.An-Nur
  • 25.Al-Furqan
  • 26.Ash-Shu`ara
  • 27.An-Naml
  • 28.Al-Qasas
  • 29.Al-`Ankabut
  • 30.Ar-Rum
  • 31.Luqman
  • 32.As-Sajdah
  • 33.Al-Ahzab
  • 34.Saba
  • 35.Faatir
  • 36.Ya-Sin
  • 37.As-Saffat
  • 38.Sad
  • 39.Az-Zumar
  • 40.Ghafir
  • 41.Fussilat
  • 42.sh-Shuraa
  • 43.Az-Zukhruf
  • 44.Ad-Dukhan
  • 45.Al-Jathiyah
  • 46.Al-Ahqaf
  • 47.Muhammad
  • 48.Al-Fath
  • 49.Al-Hujurat
  • 50.Qaf
  • 51.Adh-Dhariyat
  • 52.At-Tur
  • 53.An-Najm
  • 54.Al-Qamar
  • 55.Ar-Rahman
  • 56.Al-Waqi`ah
  • 57.Al-Hadid
  • 58.Al-Mujadila
  • 59.Al-Hashr
  • 60.Al-Mumtahanah
  • 61.As-Saf
  • 62.Al-Jumu`ah
  • 63.Al-Munafiqun
  • 64.At-Taghabun
  • 65.At-Talaq
  • 66.At-Tahrim
  • 67.Al-Mulk
  • 68.Al-Qalam
  • 69.Al-Haqqah
  • 70.Al-Ma`arij
  • 71.Nuh
  • 72.Al-Jinn
  • 73.Al-Muzzammil
  • 74.Al-Muddaththir
  • 75.Al-Qiyamah
  • 76.Al-Insan
  • 77.Al-Mursalat
  • 78.An-Naba
  • 79.An-Nazi`at
  • 80.Abasa
  • 81.At-Takwir
  • 82.Al-Infitar
  • 83.Al-Mutaffifin
  • 84.Al-Inshiqaq
  • 85.Al-Buruj
  • 86.At-Tariq
  • 87.Al-A`la
  • 88.Al-Ghashiyah
  • 89.Al-Fajr
  • 90.Al-Balad
  • 91.Ash-Shams
  • 92.Al-Layl
  • 93.Ad-Duhaa
  • 94.Ash-Sharh
  • 95.At-Tin
  • 96.Al-`Alaq
  • 97.Al-Qadr
  • 98.Al-Bayyinah
  • 99.Az-Zalzalah
  • 100.Al-`Adiyat
  • 101.Al-Qari`ah
  • 102.At-Takathur
  • 103.Al-`Asr
  • 104.Al-Humazah
  • 105.Al-Fil
  • 106.Quraysh
  • 107.Al-Ma`un
  • 108.Al-Kawthar
  • 109.Al-Kafirun
  • 110.An-Nasr
  • 111.Al-Masad
  • 112.Al-Ikhlas
  • 113.Al-Falaq
  • 114.An-Nas